Wema Asema Hampendi Tena Diamond, Hatishwi na vitisho vya Zari Staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu amesema alipokuwa akihojiwa na Sebo mtangazaji wa EFM, kwenye kipengele kiitwacho Kabali ambapo wema aliambiwa ajibu maswali kadhaa kama ndiyo au hapana na badaye kupewa nafasi ya kifafnua. Wame aliulizwa kama bado anampenda Diamond, na kama Zari ni tishio kwake kwa upande wa fasheni ambapo yote hayo Wema alijibu hapana na kijibu ndiyo alipoulizwa kama yeye ni Team Kiba. Akifafanua kuhusu kuhusu kutompenda tena Diamond Wema alisema kuwa kila kimkumbuka Diamond anamkumbuka kwa mengi mabaya . “Hapana simpendi [Diamond], yalishaisha hayo, nilishampendega, niliwahi kumpenda sana, lakini hamna tena, yaani hata sishtuki,” Wema alisema. “Nikimkumbuka Diamond most of the things ambavyo ninavikumbuka sio vitu vizuri na ndio maana hata sasa hivi imekuwa hivyo. Vizuri vilikuwepo lakini mtu anaweza akafanya vizuri akaja kufanya kimoja tu kibaya na akaharibu vyote tisa...